Back to Top
Qurani (Quran Tukufu) in Swahili Screenshot 0
Qurani (Quran Tukufu) in Swahili Screenshot 1
Qurani (Quran Tukufu) in Swahili Screenshot 2
Qurani (Quran Tukufu) in Swahili Screenshot 3
Free website generator for mobile apps; privacy policy, app-ads.txt support and more... AppPage.net

About Qurani (Quran Tukufu) in Swahili

Qurani (Qur'an) (Quran katika Kiswahili)
Tarjuma ya Qur'ani Tukufu Kwa Kiswahili

Translation of The Holy Qur'an to Swahili Language

Qur'an (kwa Kiarabu: القرآن) ni kitabu kitukufu cha Uislamu. Qur'an inatazamiwa na Waislamu kama "Neno la Allah (Mwenyezi Mungu)". Kitabu hiki kwao ni tofauti kabisa na maandiko ya vitabu vya dini nyingine kwa maana hicho kinaaminika kwamba kimeandikwa moja kwa moja na Mwenyezi Mungu, kupitia mtume wake wa mwisho, Muhammad.

Lugha na tafsiri
Imeandikwa na kusomwa kwa lugha ya Kiarabu pekee kwa zaidi ya miaka 1,400.
Kadiri ya Qurani (42:8), Mungu alimuambia Muhammad: "Na namna hivi tumekufunulia Qurani kwa Kiarabu ili uwaonye watu wa Makka na walio pembeni mwake"
Lakini, kwa vile leo Waislamu walio wengi ulimwenguni hawajui Kiarabu, maana halisi ya Qur'an hutolewa kwa lugha nyingine, hivyo kupelekea wasomaji kuelewa vyema yale maneno ya Kiarabu kwenye Qur'an yana maana gani. Vitabu hivyo ni kama kamusi kwa ajili ya Qur'an - hawavisomi hivi kama moja ya sehemu ya Quran tukufu na Waislam, ili kuwa badala ya Quran ya Kiarabu.
Waislamu wengi wanaamini kwamba tafsiri ile siyo ya Qur'an tukufu na wala siyo ya kweli; ni kopi ya Kiarabu tu iliyotolewa kwenye Qur'an ya kweli.

Waislamu wanaamini kwamba Qur'an tukufu mtume Muhammad alipewa na malaika Jibrīl kwenye pango la mlima Hira, kwa kipindi cha zaidi ya miaka ishirini na tatu hadi mauti wake ilipomfikia.
Qur'an tukufu haikuwa kitabu cha maandiko wakati wa uhai wa mtume Muhammad; iliwekwa kwa mawasiliano ya kimdomo tu. Bimaana, watu walihifadhi kichwani.
Mtume labda hakuwa anajua kusoma wala kuandika, lakini kwa mujibu wa Waislamu, swahaba wake Abu Bekr alikuwa akiandika maandiko yale juu ya kitu fulani wakati huo mtume Muhammad yu hai. Pale Abu Bekr alipokuja kuwa khalifa, ameileta Qur'an na kuwa kitabu kitakatifu.
Uthman, ambaye ni khalifa wa tatu, ameondoa vipengele ambavyo vilikuwa havihusiani na Qur'an tukufu.

Elementi, Sura, Mistari, Aya
Kuna sehemu 30 katika Qur'an, ambayo inafanya kuwa na sura 114. Kila sura ina namba tofauti ya mistari.
Kwa mujibu wa mafunzo ya Kiislam, sura 86 kati ya hizi zimeshuka mjini Makka, sura 24 kati ya hizi zimeshuka mjini Madina.
Miongoni mwa sura zilizoshushwa mjini Medina ni pamoja na Al-Baqara, Al Imran, Al-Anfal, Al-Ahzab, Al-Ma'ida, An-Nisa, Al-Mumtahina, Az-Zalzala, Al-Hadid, Muhammad , Ar-Ra'd, Ar-Rahman, At-Talaq, Al-Bayyina, Al-Hashr, An-Nasr, An-Nur, Al-Hajj, Al-Munafiqun, Al-Mujadila, Al-Hujraat, At-Tahrim, At-Taghabun, Al-Jumua, As-Saff, Al-Fath, At-Tawba, Al-Insan.

Mahusiano baina Qur'an na Biblia
Katika Qu'ran tukufu, inasomwa kwamba Wayahudi na Wakristo pia huamini Mungu wa kweli. Dini hizi pamoja na Uislamu huitwa za Abrahamu kwa sababu ya mahusiano haya.
Kuna baadhi ya kurasa za Qu'ran zinazoelezea habari za mambo ya watu wa katika Biblia. Kwa mfano watu wa katika Biblia waliotajwa kwenye Qu'ran ni pamoja na Adamu, Nuhu, Abraham, Lutu, Ismaili, Yakobo, Yosefu, Haruni, Musa, mfalme Daudi, Solomoni, Elisha, Yona, Yobu, Zakaria, Yohane Mbatizaji, Bikira Maria na Yesu.
Hata hivyo, kuna tofauti za muhimu kabisa baina ya Uislamu na toleo la Biblia katika kuelezea habari za aina moja. Kwa mfano, Qu'ran tukufu inaelezea kwamba Yesu Kristo si Mwana wa Mungu, kama jinsi Wakristo wanavyoamini; kwa Waislamu, alikuwa nabii tu, anayeheshimiwa kwa jina la Isa bin Mariamu.
Uislamu unafundisha kwamba haya yanatokea kwa sababu maandiko ya awali ya Biblia yamepotea na hivyo kuna baadhi ya watu wameyabadilisha. Lakini nje ya Qu'ran hakuna uthibitisho wa fundisho hilo.

Similar Apps

ተረትና ምሳሌ

ተረትና ምሳሌ

3.9

ጥቅሶቹን ያንብቡ እና አዳዲስ ነገሮችን ይማሩ.ለእርስዎ ነጻ እና የበይነመረብ ግንኙነት አያስፈልገዎትም.መደብ:ተረትና ምሳሌቡሄ...

ቁርአን ድምጽ Amharic Quran

ቁርአን ድምጽ Amharic Quran

5.0

ይህ መጽሐፍ የመጀመሪያው ምዕራፍ መግቢያውና ሙስሊሞች በአጠቃላይ ቁርአን ከእግዚአብሔር መጣ የሚል እምነት...

Constitution of Ethiopia (Ethi

Constitution of Ethiopia (Ethi

3.6

The current Constitution of Ethiopia, which is the supreme law of the...

Ismlar manosi - O‘zbek

Ismlar manosi - O‘zbek

0.0

Ilovada 14 mingdan ortiq ismlar va ularning ma'nolari bilan tanishishingiz.Ismlar manosi -...

Qurani (Quran Tukufu) in Swahi

Qurani (Quran Tukufu) in Swahi

4.7

Qurani (Qur'an) (Quran katika Kiswahili)Tarjuma ya Qur'ani Tukufu Kwa KiswahiliTranslation of The...

(In German) Status-Sprüche & Z

(In German) Status-Sprüche & Z

0.0

Du kannst die Sprüche Kopieren und in deinen Status einfügen oder direkt...

author
I'm so comfortable when when i reading this translation
Jamali Kinyashi
author
It's excelent and easy to use, thanks
Raphael Nyatunyi
author
It offline or?
WIKIDBOY TV
author
Faida
The Herald Broadcasting Network
author
Gooooood for every onw
Andrew Mbela
author
I like it most app
Shaban Juma