Back to Top
Quran Tukufu Screenshot 0
Quran Tukufu Screenshot 1
Quran Tukufu Screenshot 2
Quran Tukufu Screenshot 3
Free website generator for mobile apps; privacy policy, app-ads.txt support and more... AppPage.net

About Quran Tukufu

Qurani Tukufu kitabu kitukufu cha mwenyezi Mungu.

Qur'an (kwa Kiarabu: القرآن) ni kitabu kitukufu cha Uislamu. Qur'an inatazamiwa na Waislamu kama "Neno la Allah (Mwenyezi Mungu)". Kitabu hiki kwao ni tofauti kabisa na maandiko ya vitabu vya dini nyingine kwa maana hicho kinaaminika kwamba kimeandikwa moja kwa moja na Mwenyezi Mungu, kupitia mtume wake wa mwisho, Muhammad.

Lugha na tafsiri
Imeandikwa na kusomwa kwa lugha ya Kiarabu pekee kwa zaidi ya miaka 1,400.
Kadiri ya Qurani (42:8), Mungu alimuambia Muhammad: "Na namna hivi tumekufunulia Qurani kwa Kiarabu ili uwaonye watu wa Makka na walio pembeni mwake"
Lakini, kwa vile leo Waislamu walio wengi ulimwenguni hawajui Kiarabu, maana halisi ya Qur'an hutolewa kwa lugha nyingine, hivyo kupelekea wasomaji kuelewa vyema yale maneno ya Kiarabu kwenye Qur'an yana maana gani. Vitabu hivyo ni kama kamusi kwa ajili ya Qur'an - hawavisomi hivi kama moja ya sehemu ya Quran tukufu na Waislam, ili kuwa badala ya Quran ya Kiarabu.
Waislamu wengi wanaamini kwamba tafsiri ile siyo ya Qur'an tukufu na wala siyo ya kweli; ni kopi ya Kiarabu tu iliyotolewa kwenye Qur'an ya kweli.

Waislamu wanaamini kwamba Qur'an tukufu mtume Muhammad alipewa na malaika Jibrīl kwenye pango la mlima Hira, kwa kipindi cha zaidi ya miaka ishirini na tatu hadi mauti wake ilipomfikia.
Qur'an tukufu haikuwa kitabu cha maandiko wakati wa uhai wa mtume Muhammad; iliwekwa kwa mawasiliano ya kimdomo tu. Bimaana, watu walihifadhi kichwani.
Mtume labda hakuwa anajua kusoma wala kuandika, lakini kwa mujibu wa Waislamu, swahaba wake Abu Bekr alikuwa akiandika maandiko yale juu ya kitu fulani wakati huo mtume Muhammad yu hai. Pale Abu Bekr alipokuja kuwa khalifa, ameileta Qur'an na kuwa kitabu kitakatifu.
Uthman, ambaye ni khalifa wa tatu, ameondoa vipengele ambavyo vilikuwa havihusiani na Qur'an tukufu.

Elementi, Sura, Mistari, Aya
Kuna sehemu 30 katika Qur'an, ambayo inafanya kuwa na sura 114. Kila sura ina namba tofauti ya mistari.
Kwa mujibu wa mafunzo ya Kiislam, sura 86 kati ya hizi zimeshuka mjini Makka, sura 24 kati ya hizi zimeshuka mjini Madina.
Miongoni mwa sura zilizoshushwa mjini Medina ni pamoja na Al-Baqara, Al Imran, Al-Anfal, Al-Ahzab, Al-Ma'ida, An-Nisa, Al-Mumtahina, Az-Zalzala, Al-Hadid, Muhammad , Ar-Ra'd, Ar-Rahman, At-Talaq, Al-Bayyina, Al-Hashr, An-Nasr, An-Nur, Al-Hajj, Al-Munafiqun, Al-Mujadila, Al-Hujraat, At-Tahrim, At-Taghabun, Al-Jumua, As-Saff, Al-Fath, At-Tawba, Al-Insan.

Mahusiano baina Qur'an na Biblia
Katika Qu'ran tukufu, inasomwa kwamba Wayahudi na Wakristo pia huamini Mungu wa kweli. Dini hizi pamoja na Uislamu huitwa za Abrahamu kwa sababu ya mahusiano haya.
Kuna baadhi ya kurasa za Qu'ran zinazoelezea habari za mambo ya watu wa katika Biblia. Kwa mfano watu wa katika Biblia waliotajwa kwenye Qu'ran ni pamoja na Adamu, Nuhu, Abraham, Lutu, Ismaili, Yakobo, Yosefu, Haruni, Musa, mfalme Daudi, Solomoni, Elisha, Yona, Yobu, Zakaria, Yohane Mbatizaji, Bikira Maria na Yesu.
Hata hivyo, kuna tofauti za muhimu kabisa baina ya Uislamu na toleo la Biblia katika kuelezea habari za aina moja. Kwa mfano, Qu'ran tukufu inaelezea kwamba Yesu Kristo si Mwana wa Mungu, kama jinsi Wakristo wanavyoamini; kwa Waislamu, alikuwa nabii tu, anayeheshimiwa kwa jina la Isa bin Mariamu.
Uislamu unafundisha kwamba haya yanatokea kwa sababu maandiko ya awali ya Biblia yamepotea na hivyo kuna baadhi ya watu wameyabadilisha. Lakini nje ya Qu'ran hakuna uthibitisho wa fundisho hilo.

Matumizi:
-Application hii unaweza kusoma kwa lugha uitakayo kwa kubonyeza kwenye setting button, vilevile unaweza kusikiliza kwa kubonyeza play button chini.
-Ili kutumia application hii unatakiwa kuwasha Internet data(Bundle) kwenye Simu yenye network kuanzia 3G au zaidi au unaweza kutumia kwa kuunganisha na free Wi-Fi ya jirani yako.

Similar Apps

Bubble Shooter

Bubble Shooter

0.0

🔥Bubble Shooter is a free game.🔥It's a ancient puzzle and Match-Three game.As...

Wallpapers

Wallpapers

0.0

Wallpapers is free HD wallpapers and Backgrounds application with huge collection of...

Quran Tukufu

Quran Tukufu

0.0

Qurani Tukufu kitabu kitukufu cha mwenyezi Mungu.Qur'an (kwa Kiarabu: القرآن) ni kitabu...

Food Recipes

Food Recipes

0.0

Food Recipes enables you to meet 1000+ recipes around the world,which include...

Elimu

Elimu

0.0

What!, let me explain.Elimu application, its just sound another online educational resource...

Cloud Firenotes

Cloud Firenotes

0.0

What's up guys!. Cloud Firenotes is a notes taking application.Which enables ...

author
Excellent
Samwelyjr John
author
Nice app
Elias Ndagula